SHUJAA WA MAENDELEO NA USTAWI WA JAMII TANZANIA

HEKIMA NA UMOJA, USHINDI NA USHUJAA SMAUJATA

Jiunge na Mashujaa wengine Hapa

SMAUJATA

Shujaa Wa Maendeleo Na

Ustawi Wa Jamii

Bofya HapaKujiunga Na Mashujaa Wengine

Kuhusu SMAUJATA

SMAUJATA ni jumuiya ya kijamii ambayo imesajiliwa chini ya sheria ya asasi za kiraia (CAP .337 RE 2022) kwa usajili namba S.A.23969, SMAUJATA ilianzishwa na shujaa Sospeter Mosewe Bulugu mwaka 2022 kwa lengo la kuchochea mabadiliko chanya na kuleta   maendeleo endelevu kijamii na kiuchumi.

Dira ya SMAUJATA

Dira ya SMAUJATA ni kuwa na Taifa lenye kizazi huru chenye Haki na Usawa Kitakachoweza Kujitegemea na Kuzitambua na kutumia Ujuzi, Maarifa na Vipaji katika kujenga jamii yenye Maendeleo Endelevu

Dhamira Ya SMAUJATA

Dhamira Ya SMAUJATA ni Kuiwezesha na Kuijengea Jamii uwezo wa kutambua na kuiishi Misingi ya Haki na Usawa ili kutumia ujuzi, maarifa na vipaji katika kujenga jamii yenye Maendeleo Endelevu.

Imani Yetu Mashujaa

Imani ya SMAUJATA ni “HEKIMA NA UMOJA“, “USHINDI NA USHUJAA SMAUJATA

Malengo Ya SMAUJATA

i. Kushirikiana na wanajumuiya katika kuainisha fursa na changamoto zinazowakabili Pamoja na kuwaunganisha na jamii katika kuwawezesha kujiletea maendeleo kwa kutumia fursa ya sera za kisekta na mikakati yake kuinua ustawi wao na wa jamii.

ii. Kuelimisha kuelimisha wana jumuiya na jamii kuondokana na fikra, imani, mila, desturi na tamaduni zinazokinzana na maendeleo kwa kutumia semina, sanaa, warsha, makongamano, vyombo vya habari, matembezi ya amani, vipeperushi kuhusu haki, usawa, fursa na sera mbadala kwa maendeleo endelevu na kuiwezesha jamii kutekeleza haki na malezi ya mtoto.

iii. Kuratibu utekelezaji na uzingatiaji wa masuala ya jinsia katika programu na mipango ya maendeleo ya wana jumuiya na jamii nzima katika sekta mbalimbali.

iv. Kuibua, kuendeleza na kukuza vipaji vya wana jumuiya katika ujuzi, utaalamu na ubunifu ili kujenga jumuiya yenye uwezo wa kujitegemea.

v. Kushirikisha wana jumuiya, kushirikiana na serikali, wananchi na wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi katika shughuli za utoaji wa elimu na fursa za maendeleo na majanga katika jamii pamoja na kubadilishana mawazo, maoni na mbinu wezeshi ili kuishauri jamii na serikali katika kuboresha na kufanikisha vipaumbele vya ustawi na maendeleo ya jamii.

vi. Kufanya shughuli zingine zozote zinazohusu maendeleo na ustawi wa wana jumuiya na jamii kwa ujumla.

Dhana Ya Jumuiya Ya SMAUJATA

Dhana ya Jumuiya ya SMAUJATA ipo katika kupinga vikali, Kuibua na Kutokomeza aina zote za matukio au vitendo vya ukatili katika makundi mbali mbali ya jamii kupitia wananchi wazalendo na wadau mbali mbali kushiriki moja kwa moja katika maeneo yao dhidi ya vitendo hivi viovu

Kauli mbiu ya jumuiya hii imelenga kuhamasisha wananchi kila mmoja kushiriki kufanya yafuatayo:-

  1. KUELIMIKA na kuelimisha wengine kuhusiana na masuala yanayohusu ukatili ikiwa pamoja na kufahamu aina za ukatili madhara yake, hatua za kuchukua dhidi ya vitendo hivi na kufahamu ushiriki wa wananchi katika hili.
  2. KUWA MUANGALIZI WA JAMII na kuchukua hatua kwa kupaza sauti dhidi ya vitendo vya ukatili.
  3. KUSHAURI asas, wadau wa maendeleo, jamii, serikali na vyombo mbali mbali vya maamuzi katika kufanya maboresho mbali mbali ya huduma za kijamii hasa zile ambazo zikiwa hafifu zinaweza kuchochea vitendo vya kikatili

Fahamu Zaidi Kuhusu SMAUJATA

SMAUJATA ilizinduliwa rasmi mnamo Juni 16, 2022 na Mh Dorothy Gwajima (Mb) – Waziri Wa Maendeleo Ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika kitaifa Jijini Dodoma.

SMAUJATA ni kifupi cha maneno Shujaa Wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania.

SMAUJATA inaendesha kampeni huru ya kitaifa ya wananchi wazalendo wanao jitolea kuibua, kupambana na kutokomeza vitendo vya ukatili ambapo kufikia Septemba 2024 Jumla ya Watanzania 10,675 katika Mikoa yote nchini wamejiunga na Jumuiya hii.

TAARIFA

Habari Mpya

UPANGA WENYE NCHA MBILI UNAVYOTESA FAMILIA NYINGI ZA AFRIKA KARNE YA 21.

UPANGA WENYE NCHA MBILI UNAVYOTESA FAMILIA NYINGI ZA AFRIKA KARNE YA 21. Upanga wenye ncha mbili ni...

Akiamka Anawasha Data Badala ya Kuwasha Moto.

Akiamka Anawasha Data Badala ya Kuwasha Moto. MakalaNa Rachpa Tarimo. Katika zama hizi za digitali...

UONGOZI WA SMAUJATA

Shujaa Sospeter Mosewe Bulugu

Mwasisi na Kiongozi Mkuu wa Jumuiya

Shujaa Simon Ikumbo

Katibu Wa Seneti

Shujaa Winifrida Mahenye

Mkurugenzi wa Kamisheni na Utawala

Shujaa Gaudence Mnyang'ali

Mkurugenzi wa kamisheni na Utawala

Shujaa Protas Tendwa

Mkurugenzi wa kamisheni na Utawala

Shujaa Dr Magolanga Shagembe

Mkurugenzi Maendeleo Saikolojia, Jinsia na Makundi Maalumu

Shujaa Nanyorry Mwasha

Mkurugenzi wa wanachama, Uhusiano na Mahusiano ya Kimataifa

Sospeter Mosewe Bulugu

Mwasisi na Kiongozi Mkuu wa Jumuiya

Add Your Heading Text Here

Add Your Heading Text Here

Add Your Heading Text Here

MAONI YA WADAU

“Utoto wangu ulijaa unyanyasaji, kuniacha nikijihisi nimevunjika na peke yangu. Kiwewe kilionekana hakiwezi kushindika, lakini kwa msaada sahihi, nilipata nguvu ya kukishinda

“Nikiwa nakua, nilipitia unyanyasaji mkali wa kimwili na kihisia. Ulinivunja moyo na kunifanya nijihisi sina thamani. Lakini nilipofikia hatua ya kuomba msaada, nilipata mtandao wa msaada uliobadili maisha yangu.

“”Kama oc waathirika wa unyanyasaji wa watoto, sikuwahi kufikiria kwamba ningeweza kupata furaha na amani maishani mwangu. Unyanyasaji niliopitia uliacha makovu makubwa, kimwili na kihemko.”

MASWALI YA YAULIZWAYO MARA KWA MARA

Hujumlisha Hatua za ulinzi kama vile amri za zuio, Kuondolewa kutoka mazingira mabaya yenye kuchochea unyanyasaji.

Matokeo yanaweza kujumuisha mashtaka ya jinai, kifungo, na kupoteza haki za mzazi. Ukali hutegemea aina na kiwango cha unyanyasaji.

Ingawa ni jambo la kuhangaisha, kuripoti ni muhimu ili kuhakikisha usalama wa mtoto na kukomesha unyanyasaji. Mamlaka hufunzwa kushughulikia hali kama hizi kwa uangalifu.
Mamlaka itachunguza ripoti hiyo. Mtoto anaweza kuhojiwa, na mpango wa usalama utatengenezwa. Uchunguzi unaweza kuhusisha wafanyakazi wa kijamii, watekelezaji sheria na wataalamu wa matibabu.
Mnyanyasaji anaweza kuwa mtu yeyote – mzazi, jamaa, rafiki wa familia, mwalimu, mlezi, au hata mtoto mwingine.
Unyanyasaji wa watoto ni hatua yoyote ya mtu mwingine – mtu mzima au mtoto – ambayo husababisha madhara makubwa kwa mtoto. Inaweza kuwa ya kimwili, kihisia, ngono, au kutokana na kupuuzwa.
SMAUJATA ni kampeni ya kitaifa ya kupinga ukatili wa kijinsia na ukatili kwa watoto nchini Tanzania iliyoanzishwa na Sospeter Mosewe Bulugu mwaka 2022 chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu[1]. Kampeni hulenga kupinga kila aina ya ukatili, ukiwemo ukatili dhidi ya watoto.Smaujata inafanya kazi kwa kushirikiana kwa karibu na taasisi za serikali zinazohusika katika kutoa haki, ambazo ni ofisi za Ustawi wa Jamii, polisi pamoja na Takukuru, hasa upande wa rushwa ya ngono.
1. Kutambua na kutengeneza mtandao wa jamii wenye uwezo wa kupaza sauti kupinga, kupambana na kutokomeza ukatili dhidi ya Jinsia Zote Wanaume, wanawake, watoto na wazee.2. Kuelimisha na kurahisisha utambuzi na ufanyiwaji kazi wa viashiria vyote vya ukatilii kuanzia ngazi ya familia.SOMA ZAIDI

Machapisho Ya Wiki

WASHIRIKA WETU

TAKWIMU ZA MAFANIKIO

Kesi zilizoripotiwa
0
Kesi zilizosuruhishwa
0
Idadi ya Wanachama
0 +

PICHA ZA KUMBU KUMBU

UNGANA NASI

Jiunge Na Jumuiya Ya SMAUJATA